Baada ya Shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika (CAF) kusogeza mbele michuano ya CHAN inayohusisha wachezaji wa ndani, wakati wowote Bodi ya Ligi (TPLB) itatangaza kuendelea kwa mikiki mikiki ya ligi kuu ya NBC
Ligi hiyo ilisimamishwa kwa takribani miezi miwili kupisha michuano kombe la Mapinduzi pamoja na michuano hiyo ya CHAN
Msemaji wa Bodi wa Ligi Karim Boimanda amesema wamepokea taarifa ya kusogezwa mbele kwa michuano ya CHAN ambayo sasa itafanyika August 2025 hivyo wanatarajia kutangaza kuendelea kwa ratiba ya ligi kuu
"Taarifa ya CAF kuhusu kusogezwa mbele kwa michuano ya CHAN tumeipokea ambapo michuano hiyo sasa itafanyika August 2025 badala ya Februari kama ilivyopangwa awali"
"CHAN ni moja ya mashindano yaliyopelekea kusimama kwa ligi yetu hivyo kusogezwa mbele inaamisha ratiba yetu ya ligi na mashindano mengine ya ndani inaweza kuendelea, sasa tusubiri taarifa ya Bodi", alisema Boimanda
Bodi ya Ligi imetoa taarifa kuwa ligi itarejea mwanzoni mwa February 2025 ambapo mechi za viporo Yanga dhidi ya Kagera Sugar na Tabora United dhidi ya Simba zitapigwa



