Waamuzi wa Tanzania Ahmed Arajiga, Mohamed Mkono, Kassim Mpanga na Nasir Salum wameteuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika (CAFCC) kati ya RS Berkane (Morocco) dhidi ya Stellenbosch FC (Afrika Kusini) utakaochezwa Uwanja wa Berkane Januari 19, 2025
Arajiga atakuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na Mkono na Mpanga huku Nasir akiwa mwamuzi wa akiba
Arajiga ameendelea kupeperusha vyema bendera ya Tanzania upande wa waamuzi kwani ameendelea kuaminiwa na CAF kwa kupewa mechi kubwa ngazi ya klabu na timu za Taifa



