Azam Fc yawatema Bangala, Sidibe

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th January 2025


Azam Fc yawatema Bangala, Sidibe

Wakati dirisha dogo la usajili likifungwa Januari 15, Azam Fc imethibitisha kuachana na nyota wawili wa kigeni Yannick Bangala na Cheikh Sidibe

Bangala tayari amejiunga na klabu yake ya zamani AS Vita wakati Sidibe akikumbana na 'Thank You' huku akiwa bado anasaka timu ya kuendelea kuitumikia

Sidibe huenda akarejea Ivory Coast baada ya kukosa timu ndani ya ligi kuu ya NBC

Azam Fc imeongeza nyota wawili dirisha dogo Landry Zouzou beki kutoka Ivory Coast na kiungo mshambuliaji Zidane Sereri


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.