Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amewataka Wanasimba kuheshimu adhabu iliyotolewa na CAF kwa kuhakikisha hawafiki uwanja wa Benjamin Mkapa wakati mchezo kati ya Simba dhidi ya CS Constantine utakapopigwa siku ya Jumapili
Ahmed amesema CAF wametoa masharti ambayo klabu ya Simba inapaswa kuyatekeleza ili kuepuka kukumbana na adhabu kubwa





