Local,Normal News,Simba

Mashabiki msifike kwa Mkapa - Ahmed

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Jan 2025
Mashabiki msifike kwa Mkapa - Ahmed

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amewataka Wanasimba kuheshimu adhabu iliyotolewa na CAF kwa kuhakikisha hawafiki uwanja wa Benjamin Mkapa wakati mchezo kati ya Simba dhidi ya CS Constantine utakapopigwa siku ya Jumapili

Ahmed amesema CAF wametoa masharti ambayo klabu ya Simba inapaswa kuyatekeleza ili kuepuka kukumbana na adhabu kubwa

Aidha Simba imeandaa eneo maalum ambapo mashabiki wa jijini Dar es salaam wanaweza kujumuika kushuhudia mchezo huo

"Tuna kazi kubwa ya kumaliza nafasi ya kwanza kwenye kundi letu. Kama mnavyojua mchezo wetu tumezuiliwa kuingiza mashabiki kuingia uwanjani. Limekuwa tukio la kuumiza sana na wengine mpaka sasa bado hawajaamini, imetuchanganya pakubwa"

"Adhabu hii ni mechi moja ambapo tukitumikia adhabu hii vizuri mechi ya robo fainali mashabiki wataingia uwanjani. Niwambe Wanasimba tuheshimu hii adhabu, mtu yoyote hata kama ni mjanja kiasi gani wa kuingia uwanjani, niwaombe Wanasimba kukaa mbali na Uwanja wa Mkapa"

"Kuna watu ambao watakuwa wanaangalia kama tumefata utaratibu. Tuna idadi maalumu ya watu kuingia uwanjani hivyo hatazidi mtu hata mmoja. Kuna utaratibu tumepewa na CAF na sisi Simba tutaufata utaratibu huo"

"Kumekuwa na maoni mengi watu wakitaka tuweke screen kubwa kwenye uwanja wa Uhuru ili kelele zitakazopigwa ziwafikie wachezaji. Hairusiwi watu kukaa mita 1,000 kutoka uwanja wa Mkapa. Jambo hilo haliwezekani na kufanya hivyo ni kuvunja sheria"

"Asiyehusika yoyote akae mbali na Uwanja wa Mkapa, najua tunaumia hata mimi mwenyewe naumia. Kwa kuwa watu wanataka kuiona timu yao pamoja kama tulivyozoea, mdhamini wetu wa michuano ya kimataifa akaona atuandalie kitu cha kutuweka pamoja"

"Mo Cola ametutengea eneo maalumu la kukutana kuona timu yetu na eneo lenyewe ni Mwembe Yanga lililopo Temeke. Tutakuwepo pale kuanzia saa 5 asubuhi na kutakuwa na screen kubwa vibaya mno, hamjawahi kuiona"

"Kutakuwepo na burudani mbalimbali siku hiyo kama mwimbaji wa nyimbo ya Wivu ambaye ni Dj Mushizo lakini pia atakuwepo Dj Sinyorita"

"Lakini pia wiki mbili ziliopita tulizindua kampeni ya Onja na Ushinde ukinywa Mo Cola. Hivyo siku ya Jumapili Januari 19, 2025 kutakuwa na zoezi la kugawa zawadi kwa washindi na wengine watashinda pale pale"

"Mimi binafsi Jumapili sitaenda uwanjani, taenda Mwembe Yanga. Nimeshazoea kelele hivyo takuwa na Wanasimba wenzangu kufurahia," alisema Ahmed

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’