Local,Normal News,Yanga

Tutaiwashia moto MC Alger - Ramovic

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Jan 2025
Tutaiwashia moto MC Alger - Ramovic

Kocha Mkuu wa Yanga Sead Ramovic amesema hakuna matokeo mengine ambayo yatakuwa na maana kwao zaidi ya ushindi katika mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya MC Alger ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari mapema leo, Ramovic alisema ameandaa mkakati maalum wa kimbinu kuikabili MC Alger katika mchezo ambao ushindi ni matokeo ya lazima kwao

"Tunahitaji ushindi katika mchezo huo. Tunajua tunakwenda kucheza mechi ngumu dhidi ya MC Alger, tumejiandaa vyema, tumeandaa mpango wetu wa mchezo huu, tunataka kushinda ili tuwape furaha mashabiki wetu na wale wanaotuunga mkono"

"Kila mmoja anajua umuhimu wa mchezo huu, sio kwetu tu tunajua hata wapinzani wetu wanajua wanahitaji nini, nina matumaini makubwa kutokana na namna wachezaji wangu wanajitoa na kuelewa mfumo wangu, kesho tunakwenda kujitoa kwa kila iwezekanavyo"

"Tunakwenda kulipuka kama moto kuhakikisha tunaweka utawala katika mchezo huo, " alisema Ramovic

Ramovic amethibitisha atamkosa Maxi Nzengeli ambaye licha ya kuanza mazoezi na timu, bado hayuko tayari kucheza

Beki Yao Kouassi nae atakosekana akiwa amefanyiwa upasuaji wa goti na anaweza kuwa nje hadi wiki 6

Yanga inahitaji ushindi wa aina yoyote ili kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa kwa msimu wa pili mfululizo

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’