Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi January 18 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th January 2025


Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi January 18 2025

Manchester United wana matumaini ya kukamilisha makubaliano ya kumsajili mshambuliaji wa Sporting na Sweden Viktor Gyokeres, 26, licha ya nia ya Arsenal. (Independent)

The Gunners pia ni miongoni mwa klabu zinazotaka kumsajili kiungo wa kati wa Rosenborg raia wa Norway Sverre Nypan, 18. (Telegraph)

Chelsea wanamfuatilia winga wa Manchester United na Argentina Alejandro Garnacho, 20, na mshambuliaji wa Borussia Dortmund Muingereza Jamie Gittens, 20, kama malengo ya uhamisho wakati wa dirisha la Januari. (Sky Sports)

AC Milan wanakaribia kukamilisha uhamisho wa beki wa kati wa Manchester City mwenye umri wa miaka 34 raia wa Uingereza Kyle Walker. (Fabrizio Romano)

Huku usajili wa Walker ukikaribia, Milan sasa wamepunguza shauku ya kumsajili mshambuliaji wa Manchester United na England Marcus Rashford, 27. (L'Equipe)

Aston Villa wanapigiwa upatu kumsajili beki wa kulia wa Levante mwenye umri wa miaka 21 raia wa Uhispania Andres Garcia. (Relevo)

Kiungo wa kati wa Poland Jakub Moder, 25, anakaribia uhamisho wa pauni milioni 1.2 kwenda Feyenoord, licha ya kupewa mkataba mpya wa muda mrefu na Brighton. (Mail)

Mshambuliaji wa Brazil Richarlison, 27, amewaambia marafiki zake kwamba anataka kuondoka Tottenham na ameelekeza macho yake katika kuhamia ligi ya Saudi Arabia. (Football insider)

Aston Villa na Tottenham zinafikiria kumsajili beki wa kati wa AC Milan Fikayo Tomori, 27, lakini Juventus pia wana nia ya kumbakisha Muingereza huyo katika Serie A. (TBR Football)

AC Milan wamewasiliana na Chelsea kuhusu mshambuliaji wao wa Ureno Joao Felix, lakini the Blues hawana nia ya mkataba wa mkopo kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Gianlucadimarzio.com)

Mshambuliaji wa Galatasaray raia wa Ivory Coast Wilfried Zaha, 32, anatarajiwa kusitisha mkopo wake huko Lyon na kujiunga na klabu ya MLS Charlotte FC kwa mkopo wa miezi 18 badala yake. (Times)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.