Simba kusaka ushindi dhidi ya CS Constantine leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 19th January 2025


Simba kusaka ushindi dhidi ya CS Constantine leo

Kikosi cha Simba jioni ya leo kitashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili CS Constantine katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho (CAF CC)

Ni mechi ya kuilinda heshima ya Tanzania katika mashindano ya CAF, Simba ikiwa klabu pekee iliyofuzu robo fainali msimu huu

Hesabu za vijana wa kocha Fadlu Davids ni kushinda mchezo huo ili kuhakikisha wanakwenda kileleni mwa kundi A ili kupata droo rafiki katika hatua ya robo fainali

Kama Simba itamaliza nafasi ya kwanza kundi A itaanzia ugenini na kumalizia nyumbani mechi ya robo fainali

Lakini pia Mnyama atacheza dhidi ya timu iliyomaliza nafasi ya pili katika kundi jingine na hivyo kukwepa vigogo wengine watakaomaliza nafasi ya kwanza

Ni bahati mbaya kwa mashabiki mechi hiyo wataishuhudia kwenye TV kutokana na adhabu ya kufungiwa mechi moja ambayo Simba wamekumbana nayo kutoka CAF

Ni pigo kwa upande wa mashabiki lakini halitakuwa pigo kwa kikosi cha Simba kwani mechi mbili zilizopita, imepata matokeo mazuri ugenini katika mechi ambazo hakukuwa na mashabiki

Walishinda bao 1-0 Tunisia dhidi ya CS Sfaxien na kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Bravos nchini Angola


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.