Local,Normal News,Simba

Simba kusaka ushindi dhidi ya CS Constantine leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Jan 2025
Simba kusaka ushindi dhidi ya CS Constantine leo

Kikosi cha Simba jioni ya leo kitashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili CS Constantine katika mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho (CAF CC)

Ni mechi ya kuilinda heshima ya Tanzania katika mashindano ya CAF, Simba ikiwa klabu pekee iliyofuzu robo fainali msimu huu

Hesabu za vijana wa kocha Fadlu Davids ni kushinda mchezo huo ili kuhakikisha wanakwenda kileleni mwa kundi A ili kupata droo rafiki katika hatua ya robo fainali

Kama Simba itamaliza nafasi ya kwanza kundi A itaanzia ugenini na kumalizia nyumbani mechi ya robo fainali

Lakini pia Mnyama atacheza dhidi ya timu iliyomaliza nafasi ya pili katika kundi jingine na hivyo kukwepa vigogo wengine watakaomaliza nafasi ya kwanza

Ni bahati mbaya kwa mashabiki mechi hiyo wataishuhudia kwenye TV kutokana na adhabu ya kufungiwa mechi moja ambayo Simba wamekumbana nayo kutoka CAF

Ni pigo kwa upande wa mashabiki lakini halitakuwa pigo kwa kikosi cha Simba kwani mechi mbili zilizopita, imepata matokeo mazuri ugenini katika mechi ambazo hakukuwa na mashabiki

Walishinda bao 1-0 Tunisia dhidi ya CS Sfaxien na kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Bravos nchini Angola

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
30m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’