Al Hilal na MC Alger zimekata tiketi ya kucheza robo fainali ya ligi ya mabingwa baada ya kushika nafasi ya kwanza na ya pili kundi A
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano hiyo, Yanga walikosa nafasi ya kufuzu robo fainali baada ya kukosa ushindi katika mchezo dhidi ya MC Alger uliopigwa Jumamosi
AS FAR ya Morocco imefanikiwa kuongoza kundi B mbele ya Mamelodi Sundowns iliyomaliza katika nafasi ya pili
Orlando Pirates wakawaduwaza mabingwa watetezi Al Ahly kwa kuwapiga katika uwanja wao huko Misri na kuongoza kundi C huku Al Ahly wakimaliza katika nafasi ya pili
Esperance ndio vinara wa kundi D kwa faida ya H2H dhidi ya Pyramids timu zote zikimaliza makundi zikiwa na alama 13



