Mechi za makundi kombe la Shirikisho la CAF (CAF CC) zimehitimishwa jana na sasa kinachosubiriwa ni droo ya hatua ya robo fainali
Simba itaendelea kupeperusha bendera ya Tanzania hatua ya robo fainali baada ya kuongoza kundi A ikiungana na RS Berkane (Morocco), Zamalek(Misri) na USM Alger(Algeria) kama vinara wa makundi
Timu zilizofuzu katika nafasi ya pili ni CS Constantine (Algeria), Asec Mimosas (Ivory Coast), Stellen Bosch (Afrika Kusini) na Al Masry (Misri)
Katika droo ya robo fainali Simba itapangwa dhidi ya timu moja miongoni mwa tatu zilizomaliza nafasi ya pili katika kundi B,C na D
Kwa maana Simba itacheza dhidi ya Stellenbosch, ASEC au Al Masry mechi za robo fainali zikitarajiwa kupigwa mwezi March na habari njema ni kuwa Simba itaanzia ugenini na kumalizia nyumbani



