Juzi klabu ya Singida Black Stars ilitangaza kumsajili mlinda lango Amas Obasogie (22) raia wa Nigeria akitokea klabu ya Fasil Kenema ya Ethiopita
Taarifa ya Singida BS haikuishia katika utambulisho tu, bali walithibitisha kumchukua mchezaji huyo kwa makuliano maalum na klabu ya Yanga
Afisa Habari wa Klabu hiyo, Hussein Masanza alisema wameingia makubaliano maalum na Yanga kumchukua Obasogie
"Kipa huyo amesajiliwa na Yanga, lakini tumemchukua kwa makubaliano maalum, haya ni masuala ya kawaida kwenye mpira wa miguu hivyo si ajabu sana," alisema
Obasogie alikuwa akiichezea Fasil Kenema FC ya Ethiopia, ambapo pia mara kwa mara amekuwa akiitwa kuunda kikosi cha Timu ya Taifa ya Nigeria
Ni wazi Yanga imeanza mpango wa maboresho ya kikosi mapema ikiimarisha eneo la golikipa ili kumpa ushindani mlinda lango namba moja Djigui Diarra ambaye kwasasa anasaidiwa na walinda lango Aboutwalib Mshery na Aboubakar Khomein

