International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne January 21 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Jan 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne January 21 2025

Napoli inamuwania Alejandro Garnacho, Aston Villa yakataa ombi la West Ham la kumsajili Jhon Duran, Manchester United wako mbioni kumsajili Patrick Dorgu kutoka Lecce na kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti anatarajiwa kuondoka majira ya joto

Napoli wana matumaini ya kufikia mkataba wa pauni milioni 50 kumsaini winga wa Manchester United na Argentina Alejandro Garnacho, 20. (Corriere dello Sport, kwa Kiitaliano)

Ombi la West Ham la kumsajili Jhon Duran kwa pauni milioni 57 limekataliwa na Aston Villa, ambao wameamua kutomuuza mshambuliaji huyo wa Colombia mwenye thamani ya pauni milioni 80 katika kipindi hiki cha uhamisho wa wachezaji. (Telegraph - usajili unahitajika)

Manchester United wanajadiliana na beki wa Lecce Patrick Dorgu, kwa lengo la kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Denmark mwenye umri wa miaka 20 kuziba pengo katika kikosi cha Ruben Amorim. (Athletic -usajili inahitajika)

United pia imemfuatilia beki wa Wolves na Algeria Rayan Ait-Nouri, 23, na beki wa wa Crystal Palace na England Tyrick Mitchell, 25, kwa kuhofia kumkosa mlinzi wa Paris-St Germain na Ureno Nuno Mendes, 22, katika uhamisho wa wachezaji Januari hii. (ESPN)

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo majira ya kiangazi, huku kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso akipigiwa upatu kuchukua nafasi ya Muitaliano huyo. (Ondacero - kwa Kihispania)

Liverpool wanakabiliwa na mgogoro mpya wa kandarasi, huku beki wa Ufaransa Ibrahima Konate, 25, akiwa bado hajatia saini mkataba mpya na klabu hiyo licha ya kumepewa ofa mpya. (Telegraph - usajili unahitajika)

Kiungo wa Manchester City na England Jack Grealish, 29, ananyatiwa na Inter Milan na Borussia Dortmund, huku mustakabali wake Etihad ukizidi kutofahamika. (Sun)

Tottenham wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Ipswich Town Muingereza Liam Delap, 21, mwezi huu lakini huenda wakakabiliana na ushindani kutoka kwa Chelsea. (Team Talk)

Liverpool haina nia ya kupokea dau la kumuuza kiungo wa kati wa England c wa hini ya umri wa miaka 21 Harvey Elliott, 21, mwezi Januari au katika ahamisho wa majira ya kiangazi, licha ya kukosa kuchezea kikosi cha kwanza. (Football Insider)

Beki wa Hungary Milos Kerkez atasalia Bournemouth licha ya kuwaniwa na klabu ya Manchester United, lakini mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 huenda akahama wakati wa usajili wa majira ya kiangazi. (Florian Plettenberg, Sky Germany)

AC Milan wanafikiria kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Denmark wa Manchester United Rasmus Hojlund, 21, na mshambuliaji wao wa kimataifa wa Uholanzi Joshua Zirkzee, 23. (ESPN)

Juventus wamefanya mazungumzo na klabu ya Udinese kuhusu uhamisho wa beki wa Denmark Thomas Kristensen, 23, ambaye pia analengwa na Tottenham na Leicester City. (Mail)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’