Local,Normal News,Simba

Simba yapania kuendeleza ubabe Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Jan 2025
Simba yapania kuendeleza ubabe Ligi Kuu

Baada ya kukamilisha malengo ya kuongoza kundi A katika michuano ya kombe la Shirikisho (CAF CC), kocha mkuu wa Simba Fadlu Davids alitoa mapumziko ya siku nne kwa wachezaji wake

Kesho kikosi cha Simba kinatarajiwa kurejea kambini kwa ajili ya mchezo wa Kombe la FA, pamoja na Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Tabora United unaotarajiwa kupigwa Februari 2, mwaka huu, katika Uwanja Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora

Jumapili Januari 26 Simba itamenyana na TRA Kilimanjaro katika mchezo wa raundi ya pili kombe la Shirikisho la CRDB kabla ya kusafiri mkoani Tabora kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tabora United

Meneja Habari na Mawasiliano Simba, Ahmed Ally, amesema macho na hesabu zao wanazielekeza zaidi kwenye mchezo huo wa Februari 2 dhidi ya Tabora United

Ahmed amesema wanauchukuliwa kwa uzito mkubwa mchezo huo na watakwenda kwa tahadhari zote

"Tunakwenda kukabiliana na Tabora United, haitokuwa mechi nyepesi hata kidogo, lakini tutakwenda kwa ajili ya kupata matokeo mazuri"

"Sijajua ubora wa Tabora United uko wapi, ila ninachojua wanaweza kushinda michezo migumu, na kama ni hivyo hata sisi tunawajibika kwenda kwa tahadhari kubwa ili wasije kupata pia ushindi mbele yetu," alisema

Tabora United ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Yanga, Novemba 7, na kisha kulazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Singida Black Stars Novemba 25, kabla ya kuichapa Azam FC 2-1, Desemba 13, mwaka jana

Alisema kwa hali ambayo ligi imefika hawapaswi kudondosha hata pointi moja, hivyo hawako tayari kupoteza mchezo huo

"Katika ligi hii ilipofika ukiruhusu hata kupoteza pointi moja umesharuhusu mpinzani wako akufikie na kukupita kwa hiyo tunawajibika kuifunga Tabora na ni moja ya michezo migumu tuliyonayo mwezi Februari," alisema Ahmed

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’