KenGold kutambulisha kikosi kipya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd January 2025


KenGold kutambulisha kikosi kipya

Klabuu ya KenGold, Jumatano Januari 29 itafanya Tamasha la MAKARASHA DAY mkoani Mbeya ili kutambulisha wachezaji na benchi la ufundi katika uwanja wa Sokoine

Baada ya kufanya usajili mkubwa katika dirisha dogo lililofungwa Januari 15, timu hiyo imepania kujinusuru na kuteremka daraja wakianza na tukio hilo kama sehemu ya hamasa kuelekea mechi za duru ya pili zinazoanza Februari 2025

KenGold ilisajili takribani wachezaji 22 katika dirisha dogo huku pia ikileta kocha mpya Vladislav Heric raia wa Serbia

KenGold inaburuza mkiani ligi kuu ya NBC ikiwa na alama 6 na kusalia na mechi 14

Watahitaji kushinda angalau mechi 10 ili kuwa na nafasi ya kunusurika kushika daraja au kucheza play-off


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.