Klabuu ya KenGold, Jumatano Januari 29 itafanya Tamasha la MAKARASHA DAY mkoani Mbeya ili kutambulisha wachezaji na benchi la ufundi katika uwanja wa Sokoine
Baada ya kufanya usajili mkubwa katika dirisha dogo lililofungwa Januari 15, timu hiyo imepania kujinusuru na kuteremka daraja wakianza na tukio hilo kama sehemu ya hamasa kuelekea mechi za duru ya pili zinazoanza Februari 2025
KenGold ilisajili takribani wachezaji 22 katika dirisha dogo huku pia ikileta kocha mpya Vladislav Heric raia wa Serbia
KenGold inaburuza mkiani ligi kuu ya NBC ikiwa na alama 6 na kusalia na mechi 14
Watahitaji kushinda angalau mechi 10 ili kuwa na nafasi ya kunusurika kushika daraja au kucheza play-off



