Local,Normal News,Yanga

Yanga kumaliza hasira kwa Copco?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Jan 2025
Yanga kumaliza hasira kwa Copco?

Baada ya mapumziko ya siku chache, kikosi cha Yanga jana kilirejea mazoezini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kombe la Shirikisho la CRDB hatua ya 64 bora dhidi ya Copco Fc

Mchezo huo utapigwa Jumamosi, Januari 25 katika uwanja wa KMC Complex

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema baada ya kuondoshwa katika michuano ya ligi ya mabingwa, wanapaswa kukusanya nguvu ili kuhakikisha wanatetea mataji yao yote

Kamwe amesema kama watashindwa kutetea taji la Ligi Kuu na FA, maumivu yake yatakuwa makubwa kuliko maumivu waliyopata baada ya kushindwa kufuzu robo fainali CAF CL

"Tumerejea mazoezini kujiandaa na mchezo wa kombe la FA dhidi ya Copco ambao utapigwa Jumamosi uwanja wa KMC Complex"

"Mchezo huu unaonekana kama mwepesi lakini sio kweli kwani tunahitaji kufanya kazi ya ziada, tumetoka kwenye huzuni ya kushindwa kufuzu robo fainali ya CAF CL"

"Kama hatutauchukulia mchezo huu kwa umakini, mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi kwetu"

"Tuna jukumu la kutetea mataji yetu yote tukianza na hili la FA. Kama tutashindwa kutetea makombe haya basi maumivu tutakayopata ni makubwa pengine kuliko tuliyopata baada ya kushindwa kufuzu robo fainali CAF CL," alisema Kamwe

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’