Simba yapiga hodi uhamiaji

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th January 2025


Simba yapiga hodi uhamiaji

Klabu ya Simba imewaombea uraia wa Tanzania wachezaji wake 9 wa kigeni ambao hawaitwi katika timu zao za Taifa, imefahamika

Hatua imekuja siku chache baada ya klabu ya Singida Black Stars kufanikisha kupata uraia wa Tanzania kwa wachezaji wao wanne, Emmanuel Keyekeh (27) kutoka Ghana, Arthur Bada (22) kutoka Ivory Coast, Amas Obasogie (22) kutoka Nigeria na Damaro Camara (21) kutoka Guinea

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amethibitisha timu hiyo kupeleka maombi hayo Uhamiaji pia wakiomba kupewa utaratibu ili kufanikisha jambo hilo

"Ni kweli Simba imetuma maombi Idara ya uhamiaji kuomba wachezaji 9 wa Kimataifa ambao hawapati nafasi katika timu zao za Taifa ili wapewe uraia wa Tanzania. Kinachosubiriwa ni maelekezo kutoka Uhamiaji ili mchakato huo uanze mara moja," alisema Ahmed


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.