Alliance Football Club imethibitisha kifo cha James Marwa Bwire, aliyekuwa muasisi wa Alliance School Sports Academy, ambayo inamiliki timu mbili za Alliance Girls inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) na Alliance Football Club inayoshiriki First League
Taarifa hiyo imeeleza Bwire alifariki dunia usiku wa Januari 25 akiwa jijini Mwanza
Alliance Academy imeibua vipaji vya wacheza soka wengi wa kiume na wa kike wanaocheza ndani na nje ya nchi




