Lewandowski aipa ushindi muhimu Barcelona

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd February 2025


Lewandowski aipa ushindi muhimu Barcelona

Bao la Robert Lewandowski la kipindi cha pili liliihakikishia Barcelona ushindi wa 1-0 dhidi ya Deportivo Alaves Jumapili, huku wenyeji walio nafasi ya tatu wakipunguza pengo la vinara wa LaLiga Real Madrid hadi pointi nne

Huu ni shindi wa pili wa ligi kwa Barcelona katika ligi ambapo umeiwezesha kufikisha pointi 45 baada ya kucheza mechi 22, huku Alaves ikisalia nafasi ya 18 kwenye msimamo, pointi mbili chini ya mstari wa usalama

Mapema Jumamosi Real Madrid iliangukia pua kwa kuchapwa bao 1-0 na Espanyol matokeo ambayo yamewapunguza kasi licha ya kuwa mabingwa hao watetezi bado wako kileleni

"Kabla ya mchezo tulijua lazima tushinde. Tuko nyuma kwa pointi chache,” Lewandowski, mfungaji bora wa LaLiga, alisema baada ya kufunga bao lake la 18 kwenye kampeni

"Siku zote hatuwezi kushinda mabao matatu, manne au matano, wakati mwingine mechi inakuwa ngumu"

"Lakini ni soka, tulicheza kwa uvumilivu na umakini na mwisho tukafunga bao moja zaidi ya mpinzani. Tuna furaha sana."amesema.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.