Kocha Mkuu wa Yanga Sead Ramovic amesema winga aliyesajiliwa na timu hiyo katika dirisha dogo Jonathan Ikangalombo bado anaimarisha utimamu wa mwili kabla ya kuanza kuwatumikia waajiri wake hao wapya
"Ikangalombo ni mchezaji mzuri sana, kwa muda mfupi aliokuwa hapa ameonyesha ni mchezaji ambaye atatusaidia sana"
"Hata hivyo kwa sasa bado hayuko 'fit', anafanya mazoezi maalum ili kuimarisha 'fitness' yake"
"Hatutaki kuharakisha kumtumia halafu tukamsababishia madhara ikiwa ni pamoja na kuumia"
"Tunahitaji awe katika kiwango cha fitness ambacho tutajiridhisha anaweza kuanza kucheza," alisema Ramovic
Ikangalombo na Isra Mwenda walitua Yanga katika usajili wa dirisha dogo. Mwenda alijiunga na Yanga mapema zaidi hivyo kupata takribani wiki nne za mazoezi kabla ya kuanza kutumika



