Klabu ya Yanga imethibitisha kusitisha mkataba wa aliyekuwa Kocha Mkuu Sead Ramovic na Kocha Msaidizi kwa makubaliano ya pande mbili
Taarifa iliyotolewa na Yanga imemtangaza Miloud Hamdi kuwa Kocha Mkuu kuchukua nafasi ya Ramovic
Miloud ni kocha mwenye uzoefu mkubwa na soka la Afrika akiwahi kuinoa klabu ya USM Alger na kucheza fainali ya ligi ya mabingwa Afrika 2015-16
Kocha huyo anajiunga na Yanga akitokea klabu ya Singida Black Stars



