Simba imeshindwa kurudi kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo uliopigwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara
Lionel Ateba aliitanguliza Simba kwa bao la dakika ya 57 akimalizia pasi ya Ladark Chasambi
Hata hivyo Chasambi alijifunga dakika ya 75 baada ya mpira aliorudisha kwa mlinda lango Moussa Camara kumzidi nguvu na kujaa kimiani
Matokeo haya yameifanya Yanga isalie kileleni na alama 45 baada ya ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya KenGold hapo jana
Aidha matokeo ya mechi nyingine zilizopigwa mapema leo, Tanzania Prisons imeichapa Mashujaa Fc mabao 2-1 huku Dodoma Jiji ikikubali kipigo cha bao 1-0 nyumbani dhidi ya Pamba Jiji



