Simba yadondosha alama Manyara, Prisons, Pamba safi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th February 2025


Simba yadondosha alama Manyara, Prisons, Pamba safi

Simba imeshindwa kurudi kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Fountain Gate katika mchezo uliopigwa uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara

Lionel Ateba aliitanguliza Simba kwa bao la dakika ya 57 akimalizia pasi ya Ladark Chasambi

Hata hivyo Chasambi alijifunga dakika ya 75 baada ya mpira aliorudisha kwa mlinda lango Moussa Camara kumzidi nguvu na kujaa kimiani

Matokeo haya yameifanya Yanga isalie kileleni na alama 45 baada ya ushindi wa mabao 6-1 dhidi ya KenGold hapo jana

Aidha matokeo ya mechi nyingine zilizopigwa mapema leo, Tanzania Prisons imeichapa Mashujaa Fc mabao 2-1 huku Dodoma Jiji ikikubali kipigo cha bao 1-0 nyumbani dhidi ya Pamba Jiji


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.