International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Februari 08 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Feb 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Februari 08 2025

Manchester United wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Ipswich Town Liam Delap, 21, ikiwa hawataweza kumsajili mshambuliaji wa Sporting na Uswidi Viktor Gyokeres, 26, au mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 26, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Galatasaray. (GiveMeSport)

Manchester City wamedhamiria kuimarisha kikosi chao kwa ajili ya msimu ujao na wameelekeza macho yao kwa kiungo wa kati wa Atalanta na Brazil Ederson mwenye umri wa miaka 25. (Fichajes )

Mshambuliaji wa Brazil Vinicius Jr, 24, yuko kwenye mazungumzo na Real Madrid ili kuongeza mkataba wake katika klabu hiyo, ingawa makubaliano hayajakamilika. (Relevo)

Borussia Dortmund huenda ikalazimika kumuuza winga Muingereza Jamie Gittens, 20, ambaye analengwa na Liverpool, Manchester United na Chelsea, ikiwa hawatafuzu kwa Ligi ya Mabingwa msimu ujao. (Caught Offside)

&Kiungo wa kati wa Crystal Palace na Uingereza Adam Wharton, 21, na kiungo wa kati wa Southampton Muingereza Tyler Dibling, 18, ndio wanaolengwa na Tottenham. (Football Transfers)

Everton itajaribu kumsajili mshambuliaji wa West Bromwich Albion mwenye umri wa miaka 21 Tom Fellows tena msimu wa joto. (Football Insider)

The Toffees pia wanahisi wanahitaji kuimarisha kikosi katika karibu kila eneo na wameanza kubainisha malengo yao ya msimu wa joto. (i Sport)

Tottenham itazingatia mustakabali wa Ange Postecoglou kama meneja ikiwa watashindwa kuifunga Aston Villa katika Kombe la FA wikendi hii. (NipeSport)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’