Jana Pamba Jiji waliiduwaza Azam Fc katika dimba la CCM Kirumba wakiibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara
Bao lililowazamisha Azam FC lilifungwa na kiungo mkongwe, Deus David Kaseke dakika ya 86, akigusa mpira wa kwanza baada tu ya kuingia kutokea benchi kuchukua nafasi ya kiungo Mrundi, Shassir Nahimana
Ushindi huo wa pili mfululizo wakitoka kushinda ugenini dhidi ya Dodoma Jiji 1-0 pia, umeifanya Pamba Jiji FC ifikishe pointi 18 katika mchezo wa 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya 12, wakati Azam FC imbaki na pointi zake 39 za mechi 18 pia nafasi ya tatu
Katika mechi nyingine, wenyeji Namungo Fc walilazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Dodoma Jiji katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi
Mabao ya Namungo Fc yalifungwa na Pius Buswita dakika y 44 na Erasto Nyoni dakika ya 56 kwa penalti, wakati ya Dodoma Jiji walitangulia kufunga mabao yao kupitia Paul Peter dakika ya 21 na Apollo Otieno dakika ya 31
Kwa matokeo hayo, Namungo Fc wamefikisha pointi 18 katika mchezo wa 18 na kushuka kwa nafasi moja hadi ya 13, wakati Dodoma Jiji wakifikisha pointi 20 katika mchezo wa 18 na kupanda kwa nafasi mbili hadi ya nane
Mechi nyingine tatu zinapigwa leo, Ken Gold itakuwa mwenyeji wa Fountain Gate huku KMC ikiumana na Singida BS na mechi nyingine kuwakutanisha JKT Tanzania dhidi ya mabingwa watetezi, Yanga



