Local,Normal News,Dodoma

Dodoma Jiji yapata ajali Lindi

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 Feb 2025
Dodoma Jiji yapata ajali Lindi

Timu ya Dodoma Jiji imepata ajali ya basi ikitokea Ruangwa mkoani Lindi kuja jijini Dar es Salaam, baada ya jana tu kumaliza mchezo wake wa Ligi Kuu Bara dhidi ya wenyeji wao Namungo FC, uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

Katibu Mkuu wa Dodoma Jiji, Fortunatus Johnson amesema ajali hiyo imetokea katikati ya Nangurukuru na Somanga, huku akiweka wazi majeruhi ni wengi ila hakuna taarifa yoyote ya kifo hadi sasa.

"Basi lilipinduka mara mbili kwenye mto na wachezaji waliopata majeraha ya ajali ni wengi, tunashukuru tumepata msaada wa haraka sana wa kijiji na Serikali ya Mkoa wa Lindi ambao hadi muda huu tunapoongea wanaendelea kuwaokoa," amesema.

Fortunatus amesema kwa sasa ni mapema kuzungumza kile kinachoendelea ingawa baada ya muda watatoa taarifa kamili kwa kushirikiana na madaktari wa mkoa, hivyo mashabiki, wapenzi na wadau wa soka nchini waendelee kuwaombea majeruhi wote.

Dodoma Jiji ilikuwa safarini kuja Dar es Salaam kisha kwenda jijini Mbeya kwa ajili ya mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya maafande wa Tanzania Prisons uliopangwa kuchezwa Februari 14 kwenye Uwanja wa Sokoine

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
35m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’