Juzi mashabiki wa Simba waliizima kampeni ya kumchafua kinda Ladark Chasambi kibabe wakimtuza fedha baada ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Tanzania Prisons
Katika mchezo huo Chasambi alifunga moja ya mabao katika ushindi wa mabao 3-0 ambao uliirejesha Simba kileleni mwa msimamo wa ligi
Baada ya kushambuliwa sana mitandaoni baada ya kujifunga katika mchezo dhidi ya Fountain Gate, mshabiki wa Simba wameonyesha kumuunga mkonomchezaji huyo wakimpa thamani
Katika mpira wa miguu, makosa ni sehemu ya mchezo kwani kila mchezaji hukosea kwa nyakati tofauti







