Uwanja wa Kimataifa kujengwa Dodoma

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th February 2025


Uwanja wa Kimataifa kujengwa Dodoma

Jana Serikali ya Tanzania ilisaini mkataba wa ujenzi wa uwanja wa mchezo wa mpira wa miguu jijini Dodoma na mkandarasi kampuni ya LimontaI Spa ya nchini Italia wenye thamani ya zaidi ya Sh350 bilioni.

Mradi huo utatekelezwa kwa miaka miwili kuanzia sasa, huku ukitarajiwa kuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji zaidi ya 32,000 ambao ni mradi wa pili wa ujenzi wa viwanja vipya vilivyotangazwa na Serikali.

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi akishuhudia utiaji saini wa mkataba huo

Profesa Kabudi alisema mradi huo ni kielelezo cha kuendelea kuimarisha sekta ya michezo nchini.

Kusainiwa kwa mkataba huo kunaondoa sintofahamu ya muda mrefu ya ujenzi wa uwanja Dodoma kutokana na kukwama kwa ufadhili wa Serikali ya Morocco ambapo kwa sasa mradi huo utafadhiliwa na Serikali ya Tanzania kwa asilimia 100


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.