Yanga yaibamiza KMC 6-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th February 2025


Yanga yaibamiza KMC 6-1

Yanga imeendeleza ubabe katika ligi kuu ya NBC ikiichapa KMC mabao 6-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex

Stephane Aziz Ki alikuwa shujaa wa Yangaa katika mchezo huo akifunga hat-trik na kubeba tuzo ya nyota wa mchezo

Mabao mengine ya Yanga katika mchezo huo ambao waliutawala kwa muda mwingi yalifungwa na Prince Dube, Maxi Nzengeli na Israel Mwenda

Bao pekee la kufutia machozi kwa upande wa KMC lilifungwa na Redemtus Mussa

Ushindi huo umeirejesha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 49

Katika mechi nyingine zilizopigwa leo, Tabora United ililazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Ken Gold wakati Kagera Sugar ikipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Fountain Gate

Prisons wamepoteza mechi nyumbani kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Namungo Fc


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.