Simba kuifuata Namungo Fc leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th February 2025


Simba kuifuata Namungo Fc leo

Kikosi cha Simba leo Jumatatu, Februari 17 kinaelekea wilayani Ruangwa mkoani Lindi kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc

Mchezo huo utapigwa Jumatano, Februari 19 katika uwanja wa Majaliwa saa 12:30 jioni

Simba itaelekea Lndi ikiwa na kikosi chake kamili kuwania alama tatu muhimu

Baada ya kukosekana kwa wiki mbili akiwa majeruhi, kiungo mshambuliaji Kibu Denis yuko fit akiwa miongoni mwa wanaosafiri Ruangwa kuikabili Namungo Fc

Wekundu hao wa Msimbazi watakuwa na kazi mbele ya Namungo ambayo haijawahi kuwa timu nyepesi mbele ya Simba inapocheza katika uwanja wa Majaliwa

Katika misimu mitatu iliyopita, Simba haikuweza kuondoka na alama tatu Ruangwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.