Kikosi cha Simba leo Jumatatu, Februari 17 kinaelekea wilayani Ruangwa mkoani Lindi kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc
Mchezo huo utapigwa Jumatano, Februari 19 katika uwanja wa Majaliwa saa 12:30 jioni
Simba itaelekea Lndi ikiwa na kikosi chake kamili kuwania alama tatu muhimu
Baada ya kukosekana kwa wiki mbili akiwa majeruhi, kiungo mshambuliaji Kibu Denis yuko fit akiwa miongoni mwa wanaosafiri Ruangwa kuikabili Namungo Fc
Wekundu hao wa Msimbazi watakuwa na kazi mbele ya Namungo ambayo haijawahi kuwa timu nyepesi mbele ya Simba inapocheza katika uwanja wa Majaliwa
Katika misimu mitatu iliyopita, Simba haikuweza kuondoka na alama tatu Ruangwa



