Local,Normal News,Yanga, Singida

Yanga mikononi mwa Singida BS ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
17 Feb 2025
Yanga mikononi mwa Singida BS ligi kuu

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi za mzunguuko wa 20 zitaunguruma

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga, watakuwa uwanja wa nyumbani KMC Complex kumenyana na Singida Black Stars katika mchezo unaotarajiwa kuwa na upinzani mkali

Mechi kati ya Yanga dhidi ya Singida Black Stars haijawahi kuwa nyepesi. Mara ya mwisho timu hizo zilipokutana katika mchezo wa duru ya kwanza uliopigwa visiwani Zanzibar, Yanga iliibuka na ushindi wa bao 1-0, bao pekee likifungwa na Pacome Zouzoua

Singida BS wametoka kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, uwanja ambao Yanga ilidondosha alama mbili dhidi ya maafande hao

Lakini pia Wananchi wametoka kuichabanga KMC mabao 6-1, KMC pia waliichapa Singida BS mabao 2-0 hapo KMC Complex

Hivyo ni mchezo utakaozikutanisha timu 'zilizojisahihisha' baada ya kutofanya vizuri katika mechi zilizotangulia

Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi anakwenda kukabiliana na waliokuwa waajiri wake ambao alidumu nao kwa takribani siku 36

Yanga imekuwa na rekodi ya kibabe katika dimba la KMC Complex, ni wazi Singida BS watakumbana na aina tofauti ya soka kulinganisha na vile walivyocheza mara ya mwisho Zanzibar

Mchezo mwingine unaopigww jioni ya leo ni kati ya Fountain Gate dhidi ya Tabora United uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’