Droo ya mechi za robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL) na kombe la Shirikisho (CAF CC) inafanyika leo huko Doha, Qatar
Wababe 16 wa soka Afrika leo ndio watawajua wapinzani wao katika mechi za robo fainali
Afrika Mashariki na Kati itawakilishwa na Simba, klabu pekee iliyoting robo fainali katika ukanda huo
Mnyama aliongoza kundi A kombe la Shirikisho, leo atamfahamu mpinzani wake kuelekea mechi ya robo fainali
Timu zilizomaliza nafasi ya pili kundi B, C na D mojawapo ndio itakayomenyana na Simba
Inaweza kuwa Stellenbosch ya Afrika Kusini, Asec Mimosa ya Ivory Coast au Al Masry ya Misri
Simba itaanzia ugenini mechi ya kwanza ya robo fainali na kumalizia nyumbani mechi ya pili



