Droo ya robo fainali CAF ni leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 20th February 2025


Droo ya robo fainali CAF ni leo

Droo ya mechi za robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL) na kombe la Shirikisho (CAF CC) inafanyika leo huko Doha, Qatar

Wababe 16 wa soka Afrika leo ndio watawajua wapinzani wao katika mechi za robo fainali

Afrika Mashariki na Kati itawakilishwa na Simba, klabu pekee iliyoting robo fainali katika ukanda huo

Mnyama aliongoza kundi A kombe la Shirikisho, leo atamfahamu mpinzani wake kuelekea mechi ya robo fainali

Timu zilizomaliza nafasi ya pili kundi B, C na D mojawapo ndio itakayomenyana na Simba

Inaweza kuwa Stellenbosch ya Afrika Kusini, Asec Mimosa ya Ivory Coast au Al Masry ya Misri

Simba itaanzia ugenini mechi ya kwanza ya robo fainali na kumalizia nyumbani mechi ya pili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.