Klabu ya Namungo FC imepanga kukata rufaa kuhusu kadi nyekundu ya mlinzi wao raia wa Burundi, Derrick Mukombozi, ambaye alipewa hapo jana katika mchezo wao dhidi ya Simba
Namungo ilikubali kichapo cha mabao 3-0 katika mchezo ambao ulishuhudiwa matukio mengi yenye utata ikiwa ni pamoja na kadi nyekundu hiyo
Katika mahojiano na Crown Fm, Mukombozi alikanusha madai ya kumpiga mchezaji wa Simba (Lionel Ateba) au kumtukana mwamuzi na hakuelewa kwa nini alipewa kadi nyekudnu
"Binafsi namshukuru Mungu,ila sijui kwanini mwamuzi alinionyesha kadi nyekundu,mimi sikumtukana mtu wala sikumpiga mtu,halafu nilimuuliza refa Kama nimempiga Ateba mbona hukuweka penalty?," alihoji Mukombozi



