Local,Normal News,Yanga, Pamba

Kocha Yanga alia na uwanja wa CCM Kirumba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Mar 2025
Kocha Yanga alia na uwanja wa CCM Kirumba

Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amewapongeza wachezaji wake kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa CCM Kirumba jana

Licha ya ushindi huo, Hamdi amesema wachezaji wake walipata wakati mgumu kukabiliana na hali ya eneo la kuchezea la uwanja wa CCM Kirumba

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa ushindi huu muhimu lakini niseme wazi, uwanja haukuwa rafiki upande wetu"

"Ukiwa mbali unaweza kudhani uwanja huu uko katika hali bora lakini nikwambie haikuwa rahisi hata kutuliza mpira"

"Utaona kipindi cha kwanza wachezaji wangu walipata wakati mgumu lakini nafurahi kipindi cha pili baada ya kufanya mabadiliko tulitulia na tumeweza kupata ushindi"

"Alama tatu za mchezo huu ni muhimu sana kwetu katika kukamilisha malengo yetu. Niwapongeze mashabiki wa Yanga waliokuja kwa wingi uwanjani kutuunga mkono. Mashabiki wameendelea kunishangaza niwapongeze kwa kile wanachofanya kwa timu yao," alisema Hamdi

Mabao ya Yanga katika mchezo huo yalifungwa Stephane Aziz Ki aliyepachika mabao mawili na Chadrack Boka aliyefunga bao lake kupitia mpira wa faulo

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’