Fadlu aipigia hesabu kali Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th March 2025


Fadlu aipigia hesabu kali Yanga

Mkufunzi wa Simba Fadlu Davids amesema maandalizi ya mchezo dhidi ya Yanga yamekamilika na wako tayari kwa mchezo huo

Akizungumza katika mkutano na wanahabari, Fadlu amesema ari na morali ya wachezaji kuelekea mchezo huo iko juu na kila mmoja 'akiutaka mchezo'

"Tumekuwa na wakati mzuri wa kujiandaa na mchezo huu. Ari ya wachezaji iko juu kila mchezaji anaonyesha utayari wa kutumika katika mchezo huo"

"Tutamkosa Mzamiru Yassin ambaye ni majeruhi, tutakuwa na vipimo vya mwisho kwa wachezaji Moussa Camara na Che Malone Fondoh kuona kama watatumika lakini wachezaji wengine wote wako tayari"

"Tunajua itakuwa mechi ngumu, ni lazima tuwe katika ubora na kuhakikisha hatufanyi makosa kuwanufaisha wapinzani wetu na pia kutumia vyema nafasi"

"Hatutabadili aina yetu ya uchezaji, tunahitaji kumiliki mchezo na kufanya pressing na kuwaheshimu wapinzani wetu wanapokuwa na mpira. Tunakwenda katika mchezo huu tukiwa bora zaidi pengine kuliko mechi zilizopita dhidi ya Yanga msimu huu"

"Kipeke, nawashukuru mashabiki wetu kwa kutusapoti msimu huu, wamekuwa msaada mkubwa kwetu, nawaahidi hio kesho wataiona timu yao ikijitoa kwa asilimia zote na kuonyesha ubora pia kucheza kwa kasi sahihi kwa muda wote wa mchezo," alisema Fadlu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.