Kocha Mkuu wa Yanga Miloud Hamdi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo utakaopigwa saa 1:15 usiku, Hamdi amesema anaiheshimu klabu ya Simba na hii ni mechi kubwa lakini anaamini ubora wa timu yake unakwenda kuamua mchezo huo





