TPLB yabadili msimamo, yaahirisha Dabi ya Kariakoo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th March 2025


TPLB yabadili msimamo, yaahirisha Dabi ya Kariakoo

Kufuatia mfululizo wa matukio ambayo yalipelekea klabu ya Simba kushindwa kufanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa jana, Bodi ya Ligi imetangaza kuahirishwa mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga dhidi ya Simba ambao ulipaswa kupigwa leo katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Taarifa iliyotolewa na Bodi mapema leo imebainisha kuwa kwa sasa Kamati inapitia ushahidi mbalimbali wa matukio yaliyojiri jana usiku kabla ya kutoa maamuzi ya kilichojitokeza

Aidha Bodi imetangaza kuahirisha mchezo huo na sasa utapangiwa tarehe nyingine

Simba ilitangaza msimamo wake mapema kutoshiriki mchezo huo hadi pale wale walioihujumu Simba kuchukuliwa hatua


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.