Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeufungia uwanja wa Benjamin Mkapa kwa muda kutokana na eneo la kuchezea 'pitch' kupungua ubora wake
Kulingana na taarifa iliyotolewa na TFF, uwanja huo unatakiwa kufanyiwa maboresho ya haraka ili kuepuka kufungiwa kwa muda mrefu
Mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho (CAF CC) kati ya Simba dhidi ya Al Masry umepangwa kupigwa April 09 katika uwanja huo
Hata hivyo CAF imeiagiza TFF kutuma uwanja mbadala ambao Simba inaweza kutumia katika mchezo huo ikitokea uwanja wa Mkapa hautakuwa tayari




