Wakati hatma ya beki kisiki Che Fondoh Malone ikiwa bado mikononi mwa madaktari wanaomtibu, beki aliyeziba nafasi yake Chamou Karaboue amesema hakuna kitakachoharibika kwani yeye na Abdulrazak Hamza wataendelea kuilinda ngome ya Simba
Che Fondoh alipata majeraha katika mchezo dhidi ya Azam Fc, kuna taarifa kuwa aina ya majeraha ambayo yanamkabili Che Fondoh, huenda yakamuweka nje kwa muda mrefu zaidi kinyume na vile ilivyotarajiwa
Chamou amesema sasa ameshaizoea ligi kuu ya NBC na hivyo anafahamu vyema jinsi ya kukabiliana na washambuliaji wa timu pinzani
Amesema maelewano na Abdulrazack Hamza ni mazuri kwani muda mwingi aliokuwa akipata nafasi alicheza nae na hata Che Malone, hivyo alihitaji muda wa kumuelewa zaidi na ameupata.
"Ukuta wetu upo imara kuhakikisha hatutoki kwenye njia ya malengo yetu tuliyojiwekea, nacheza kwa maelewano mazuri na mabeki wenzangu kwa sababu nimeshawasoma"
"Ukizingatia viungo wetu wa juu ni watu wanaojua kutupunguzia presha hivyo nataka kutumia mechi hizi ambazo Che Malone hatakuwepo uwanjani kuthibitisha kwamba mimi ni beki sahihi kuitumikia Simba," alisema Chamou
Tangu Che Malone apate majeraha na nafasi yake kuchukuliwa na Chamou, Simba imecheza mechi tatu na kushinda zote pasipo kuruhusu bao



