Serikali ya Tanzania imelialika Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) kufanya ukaguzi wa uwanja wa Benjamin Mkapa baada ya kukamilika kwa maboresho
Wiki iliyopita CAF ilitangaza kuufungia uwanja wa Benjamin Mkapa kwa muda ili ufanyiwe maboresho katika eneo la kuchezea 'pitch'
Baada ya tamko la CAF, Serikali ilitoa ufafanuzi kuwa CAF walifanya ukaguzi wakati uwanja huo ukiwa katika maandalizi ya kutumika katika mchezo wa ligi kuu kati ya Azam Fc dhidi ya Simba na kuwa nyasi zake zilipunguzwa kufika chini zaidi
Akizungumza katika Mkutano na waandishi wa Habari jana, Katibu Mkuu Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo na Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa alisema uwanja huo uko tayar huku akiwatoa hofu mashabiki wa klabu ya Simba kuwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Al Masry utapigwa katika uwanja huo
"Maboresho yaliyoagizwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) yamekamilika. Tumewaalika CAF waje wafanye ukaguzi. Tuna matumaini mechi ya robo fainali Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba na Al-Masry itapigwa uwanja wa Benjamini Mkapa," alisema
CAF iiagiza TFF kutafuta uwanja mwingine ambao Simba itautumia katika mchezo huo ikitokea dimba la Mkapa halitakidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni za CAF



