Local,Transfer News,Tabora

Kiazayidi aikacha Tabora United, yaleta kocha Mzimbabwe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Mar 2025
Kiazayidi aikacha Tabora United, yaleta kocha Mzimbabwe

Uongozi wa Tabora United, umefikia makubaliano ya kuachana na kocha mkuu wa timu hiyo, Anicet Kiazayidi huku nafasi yake ikichukuliwa na Mzimbabwe, Genesis Mangombe

Haijafahamika sababu za kuvunjwa kwa mkataba wa kocha huyo raia wa DR Congo ambaye hivi karibuni alirejea nchini kwao kwa ajili ya kufanya kozi ya refresh

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Tabora United, kimebainisha kuwa uongozi wa timu hiyo na kocha huyo wamefikia makubaliano ya pande zote mbili kuvunja mkataba

"Siwezi kuzungumza sababu za kuachana na kocha aliyepita ambaye ameisaidia timu yetu kuwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo hadi sasa, ninachoweza kusema ni makubaliano ya pande zote mbili"

"Hata tuliyemleta ni kocha mzuri, hivyo tunaamini atatuvusha katika malengo yetu kwa msimu huu kwani tunatamani kumaliza nafasi za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu," alisema mtoa taarifa huyo

Alipotafutwa Kocha Kiazayidi kuzungumzia suala hilo, alisema amefikia uamuzi huo kwa makubaliano ya pande mbili, huku akisita kueleza wazi kwa kina sababu zilizomfanya kuondoka ndani ya timu hiyo

Kwa upande wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tabora United, Charles Obiny alisema kuna taratibu za kiuongozi zinaendelea juu ya hilo na zitakapokamilika wataweka wazi, hivyo mashabiki na wadau wa timu hiyo waendelee kuwapa sapoti kwa michezo ijayo

Tabora United ilimchukua Kiazayidi Novemba 2024 kuziba nafasi ya Mkenya Francis Kimanzi aliyeondolewa baada ya timu hiyo kuwa na mwenendo mbaya katika Ligi Kuu Bara msimu huu

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’