Kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Morocco usiku wa kuamkia leo Jumatano March 26, kimevuruga hesabu za timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kufuzu kwa michuano ya kombe la Dunia 2026
Aidha, ushindi huo kwa Morocco umeifanya kuwa timu ya kwanza barani Afrika kukata tiketi ya kushiriki kombe la Dunia mwakani huko Marekani
Stars ilikuwa na kipindi cha kwanza bora ikicheza kwa tahadhari na kufanikiwa kuwadhibiti Morocco licha ya presha kubwa waaliyoweka langoni kwa Tanzania
Hata hivyo mambo hayakwenda vyema mwanzoni mwa kipindi cha pili Morocco wakifanikiwa kufunga mabao yao dakika ya 51 na 58 kupitia mkwaju wa penati
Unaweza kusema ubora wa Morocco na uzoefu wao umewapa matokeo mazuri katika mchezo huo huku Stars ikiondoka na somo jingine
Morocco imefikisha alama 15 baada ya kushinda mechi zote 5 walizocheza huku Stars ikisalia nafasi ya tatu na alama 6
Vinara wa makundi wanafuzu moja kwa moja wakati timu nyingine nne zitafuzu kupitia 'best looser'



