Stars yakubali kichapo mbele ya Morocco

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th March 2025


Stars yakubali kichapo mbele ya Morocco

Kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Morocco usiku wa kuamkia leo Jumatano March 26, kimevuruga hesabu za timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kufuzu kwa michuano ya kombe la Dunia 2026

Aidha, ushindi huo kwa Morocco umeifanya kuwa timu ya kwanza barani Afrika kukata tiketi ya kushiriki kombe la Dunia mwakani huko Marekani

Stars ilikuwa na kipindi cha kwanza bora ikicheza kwa tahadhari na kufanikiwa kuwadhibiti Morocco licha ya presha kubwa waaliyoweka langoni kwa Tanzania

Hata hivyo mambo hayakwenda vyema mwanzoni mwa kipindi cha pili Morocco wakifanikiwa kufunga mabao yao dakika ya 51 na 58 kupitia mkwaju wa penati

Unaweza kusema ubora wa Morocco na uzoefu wao umewapa matokeo mazuri katika mchezo huo huku Stars ikiondoka na somo jingine

Morocco imefikisha alama 15 baada ya kushinda mechi zote 5 walizocheza huku Stars ikisalia nafasi ya tatu na alama 6

Vinara wa makundi wanafuzu moja kwa moja wakati timu nyingine nne zitafuzu kupitia 'best looser'


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.