Local,Normal News,Simba

Simba ni do or die huko Misri

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Mar 2025
Simba ni do or die huko Misri

Jumatano April 02 katika uwanja wa Suez ulioko Mji wa Ismailia, wawakilishi pekee wa Tanzania waliobaki katika michuano ya CAF, Simba watatupa karata muhimu kuikabili Al Masry katika mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC)

Ni mechi ngumu lakini muhimu sana kwa Simba ugenini, kwani mechi hii inabeba hatma ya Mnyama kuvuka hatua ya robo fainali ambayo wamekwama kwa takribani misimu mitano mfululizo katika mashindano ya CAF

Al Masry ni moja ya timu ngumu katika michuano ya kombe la Shirikisho msimu huu licha ya kuwa walimaliza nafasi ya pili katika hatua ya makundi nyuma ya Zamalek iliyoongoza kundi D

Timu hiyo ambayo inashika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu ya Misri ilipoteza mechi moja tu hatua ya makundi

Rekodi za Al Masry katika ligi ya ndani zinaonyesha kuwa mchezo wa mwisho walitoka sare 1-1 na timu ya National Bank of Egypt

Kwenye mechi sita za makundi Masry, ilishinda mechi mbili nyumbani dhidi ya Black Bulls ya Msumbiji (3-1) na Enyimba ya Nigeria (2-0) kisha ikatoa sare tatu na kupoteza mmoja dhidi ya Zamalek (1-0)

Katika mechi tano zilizopita kwenye mashindano yote Al Masry wamelazimishwa sare tatu, kushinda moja na kupoteza moja

Hata hivyo wanakutana na Simba iliyo katika kiwango bora ikitoka kushinda mechi nne kati ya tano zilizopita

Simba inanolewa na kocha Fadlu Davids ambaye ana uzoefu wa kucheza mechi hizi za mtoano

Msimu wa 2021/22 Fadlu aliiongoza Orlando Pirates kucheza fainali ya kombe la Shirikisho ambapo katika mchezo wa robo fainali aliiondosha timu yake ya sasa Simba kwa mikwaju ya penati baada ya matokeo ya jumla ya sare ya bao 1-1

Msimu huu Simba imeweka malengo makubwa ya kucheza fainali ya michuano hiyo, ushindi au hata sare huko Misri itakuwa hatua moja muhimu kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, April 09

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’