Jeshi la Polisi Tanzania limethibitisha kumshikilia Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe kwa tuhuma za kuwachafua viongozi wa Serikali
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Richard Abwao amethibitisha kwamba, Kamwe anashikiliwa tangu Jana usiku, kwa tuhuma hizo. Abwao amesema bado Kamwe yuko kizuizini akiendelea na mahojiano juu ya tuhuma hizo ambapo taarifa zaidi zitatolewa baadaye
Kamwe alikamatwa jana baada ya mchezo kati ya Tabora United dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa Ali Hassan Mwinyi na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-0
Kuelekea mchezo huo kuliibuka kupishana kauli kati yake na Mh. Paul Matiko Chacha Mkuu wa Mkoa Tabora. Hata hivyo wawili hao walionekana kusalimiana na kufurahi pamoja kabla ya mchezo
