Inaelezwa uongozi wa Simba umetenga Tsh Milioni 500 za bonasi ya wachezaji iwapo watashinda dhidi ya Al Masry na kufuzu nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC)
Mabosi wa Simba wanaongoza hamasa kuelekea mchezo huo utakaopigwa kesho Jumatano, April 09 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Jana mabosi wa Simba walishuhudia mazoezi yaliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, yakiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo huo
Mtendaji Mkuu Zubeda Sakuru, Mwenyekiti Murtaza Mangungu na Mjumbe wa Bodi wa Wakurugenzi Salim Abdallah 'Try Again' waliongoza msafara wa vigogo hao wa Simba ambao pamoja na mambo mengine wlipata nafasi ya kuzungumza na wachezaji






