Mabosi Simba waongoza hamasa kuizima Al Masry

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th April 2025


Mabosi Simba waongoza hamasa kuizima Al Masry

Inaelezwa uongozi wa Simba umetenga Tsh Milioni 500 za bonasi ya wachezaji iwapo watashinda dhidi ya Al Masry na kufuzu nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC)

Mabosi wa Simba wanaongoza hamasa kuelekea mchezo huo utakaopigwa kesho Jumatano, April 09 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Jana mabosi wa Simba walishuhudia mazoezi yaliyofanyika uwanja wa Benjamin Mkapa, yakiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo huo

Mtendaji Mkuu Zubeda Sakuru, Mwenyekiti Murtaza Mangungu na Mjumbe wa Bodi wa Wakurugenzi Salim Abdallah 'Try Again' waliongoza msafara wa vigogo hao wa Simba ambao pamoja na mambo mengine wlipata nafasi ya kuzungumza na wachezaji


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.