Serikali imetangaza kufunga kwa muda uwanja wa Benjamin Mkapa ili kupisha marekebisho katika eneo la kuchezea 'pitch'
Uwanja huo awali ulifungwa kwa ajili ya ukarabati wa eneo hilo na kufunguliwa baada ya CAF kujiridhisha na marekebisho yaliyofanyika, Simba ikiruhusiwa kutumia katika mchezo dhidi ya Al Masry
Hata hivyo mvua iliyonyesha ni kama ilichangia hali ya uwanja huo kuwa mbaya ingawa pia kulionekana mangungufu ya maji kukaa katika eneo la kuchezea
Jitihada za kuondoa maji zilifanyika kabla ya mchezo kuanza hata hivyo kuendelea kwa mvua wakati mchezo ukiendelea kulichangia eneo la kuchezea kuharibika zaidi
Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa amesema uwanja huo umefungwa kwa muda mfupi na utafunguliwa tena baada ya maboresho kukamilika



