Uwanja wa Mkapa wafungwa tena kwa muda

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th April 2025


Uwanja wa Mkapa wafungwa tena kwa muda

Serikali imetangaza kufunga kwa muda uwanja wa Benjamin Mkapa ili kupisha marekebisho katika eneo la kuchezea 'pitch'

Uwanja huo awali ulifungwa kwa ajili ya ukarabati wa eneo hilo na kufunguliwa baada ya CAF kujiridhisha na marekebisho yaliyofanyika, Simba ikiruhusiwa kutumia katika mchezo dhidi ya Al Masry

Hata hivyo mvua iliyonyesha ni kama ilichangia hali ya uwanja huo kuwa mbaya ingawa pia kulionekana mangungufu ya maji kukaa katika eneo la kuchezea

Jitihada za kuondoa maji zilifanyika kabla ya mchezo kuanza hata hivyo kuendelea kwa mvua wakati mchezo ukiendelea kulichangia eneo la kuchezea kuharibika zaidi

Msemaji wa Serikali Gerson Msigwa amesema uwanja huo umefungwa kwa muda mfupi na utafunguliwa tena baada ya maboresho kukamilika


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.