Simba yaipeleka Stellenbosch New Amaan Complex

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th April 2025


Simba yaipeleka Stellenbosch New Amaan Complex

Klabu ya Simba itatumia uwanja wa New Amaan Complex katika mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumapili April 20, saa 10 jioni

Imeelezwa uwanja wa Benjamin Mkapa ambao mchezo huo ulipaswa kupigwa bado uko katika maboresho ya eneo la kuchezea 'pitch'

Uwanja wa Amaan ulipitishwa CAF kutumika katika mashindano ya Shirikisho hilo baada ya kufanyiwa maboresho

Eneo lake la kucheza lilifanyiwa maboresho makubwa kwa kuondoa nyasi bandia na kupanda nyasi asili


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.