Yanga imetinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho la CRDB kibabe kwa ushindi wa mabao 8-1 dhidi Stand United
Unaweza kusema Yanga leo ilikuwa na mazoezi ya kutengeneza nafasi ya kufunga pengine Wananchi wangeweza kufunga mabao zaidi
Baada ya majeraha ya hapa na pale, Stephane Aziz Ki leo amerejea kikosini kikamilifu akifanikiwa kufunga mabao manne huku Clatous Chama akiendeleza ubora wake akiweka kambani mabao mawil
Nickson Kibabage na Kennedy Musonda nao waliingia kambani katika mchezo huo ambao waliweka rekodi ya kufunga mabao mengi katika michuano hiyo msimu huu
Yanga sasa itachuana na JKT Tanzania katika mchezo wa nusu fainali huku watani zao Simba wakimenyana na Singida Black Stars



