Local,Normal News,Simba

Simba yapewa nafasi kubwa kutinga fainali CAF CC

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Apr 2025
Simba yapewa nafasi kubwa kutinga fainali CAF CC

Kikosi cha Simba leo kinaelekea Zanzibar kukamilisha maandalizi ya mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini utakaopigwa Jumapili, April 20 dimba la New Amaan Complex

Simba SC wataingia kwenye nusu fainali hii wakiwa na uzoefu mkubwa katika mashindano ya Afrika na rekodi nzuri wakiwa nyumbani

Miamba hao wa Msimbazi wamekuwa wakifanya vizuri kwenye mashindano ya CAF, na kucheza Zanzibar ni kama nyumbaniΒ 

Katika michuano hiyo msimu huu, ikiwa na kikosi chenye wachezaji wengi wenye damu changa wanaonolewa na kocha raia wa Afrika Kusini Fadlu Davids, Simba ni miongoni mwa timu zinazopewa nafasi ya kutwaa ubingwa

Stellenbosch FC, maarufu kama "Stellies", wanacheza nusu fainali yao ya kwanza kabisa kwenye Kombe la Shirikisho. Nao safari yao imekuwa ya kuvutia, wakivuka hatua mbalimbali kwa kuwatoa vigogo wa soka barani Afrika. Ulinzi wao madhubuti na mashambulizi ya kushtukiza yamekuwa silaha yao kubwa

Kwa kuzingatia uzoefu wa Simba SC na faida ya kucheza nyumbani, wanapewa nafasi kubwa ya kushinda mkondo wa kwanza

Hata hivyo ni wazi itakuwa mechi yenye ushindani, Stellenbosch FC ni timu isiyotabirika – ina nidhamu ya hali ya juu na wamedhihirisha wanaweza kufanya maajabu kama waliyofanya Misri kwa kuwatoa mabingwa watetezi Zamalek katika mchezo wa robo fainali

CAF tayari imemtangaza refa mzoefu Jean Jacques Ndala kutoka DR Congo ndiye amepangwa kuchezesha mechi hiyo ya kwanza nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika

Ngambo mwenye umri wa miaka 37, amewahi kuichezesha Simba katika mechi nne tofauti za kimataifa ambapo imeshinda mbili, imetoka sare moja na kupoteza moja

Mechi ya kwanza kwa Ngambo kuichezesha Simba ilikuwa ni ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2018/2019 ambao ilipoteza kwa mabao 2-0 mbele ya JS Saoura ya Algeria ugenini

Refa huyo akachezesha mechi ya raundi ya kwanza ya ligi ya mabingwa Afrika msimu wa 2021/2022 ambayo Simba ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana.

Msimu huohuo, Ndala alichezesha mechi ya nyumbani ya hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika ambayo Simba ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya RS Berkane ya Morocco.

Mchezo wa mwisho kwa Ndala kuichezesha Simba ulikuwa ni ugenini wa mashindano ya African Football League ambao Simba ililazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Al Ahly ya Misri.

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
3m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
32m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’