Kikosi cha Simba leo kinaelekea Zanzibar kukamilisha maandalizi ya mchezo wa mkondo wa kwanza nusu fainali ya kombe la Shirikisho dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini utakaopigwa Jumapili, April 20 dimba la New Amaan Complex
Simba SC wataingia kwenye nusu fainali hii wakiwa na uzoefu mkubwa katika mashindano ya Afrika na rekodi nzuri wakiwa nyumbani





