Jumapili hii, tarehe 20 Aprili 2025, mashabiki wa soka barani Afrika watashuhudia mechi mbili za nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF. Timu nne kutoka kanda tofauti za Afrika zitachuana kuwania nafasi ya kucheza fainali ya michuano hii ya pili kwa ukubwa barani
Simba SC ya Tanzania itakuwa mwenyeji wa Stellenbosch FC ya Afrika Kusini katika uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar
Simba walimaliza hatua ya makundi wakiwa vinara wa Kundi A kwa alama 13, wakipita CS Constantine ya Algeria kwa pointi moja. Ushindi wao wa 2-0 dhidi ya Constantine katika mechi ya mwisho ya kundi uliwapa motisha kubwa kuelekea hatuaya robo fainali ambako walifanikiwa kuitupa nje ya mashindano Al Masry kwa mikwaju ya penati baada ya matokeo ya aggregate ya sare ya mabao 2-2
Kwa upande mwingine, Stellenbosch FC walimaliza nafasi ya pili katika Kundi B nyuma ya RS Berkane ya Morocco. Wakiwa katika msimu wao wa kwanza wa kushiriki michuano ya CAF, Stellenbosch wameonyesha uwezo mkubwa, ikiwa ni pamoja na ushindi wa 1-0 dhidi ya mabingwa watetezi Zamalek na kuwatupa nje ya michuano hiyo hatika hatua ya robo fainali
Mechi hii inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku Simba wakitumia uzoefu wao katika michuano ya Afrika na faida ya uwanja wa nyumbani, wakati Stellenbosch wakilenga kuendeleza mafanikio yao katika msimu wao wa kwanza kushiriki mashindano ya CAF
Katika nusu fainali nyingine, RS Berkane ya Morocco itawakaribisha CS Constantine ya Algeria. RS Berkane walimaliza hatua ya makundi wakiwa na rekodi ya asilimia 100 ya ushindi katika Kundi B, wakifunga mabao 7 na kuruhusu 2 pekee
Waliitoa Asec Mimosas ya Ivory Coast kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-o ikishinda 1-0 nyumbani na ugenini
Uzoefu wao katika michuano hii, ikiwa ni pamoja na kutwaa taji mara mbili, unawafanya kuwa miongoni mwa timu zinazopigiwa upatu kutwaa ubingwa msimu huu
CS Constantine walimaliza nafasi ya pili katika Kundi A nyuma ya Simba SC, wakiwa na alama 12. Ushindi wao wa 4-0 dhidi ya Bravos do Maquis ulionyesha uwezo wao mkubwa wa kushambulia
Katika robo fainali wakafanikiwa kuwaondoa majirani zao USM Alger kwa ushindi wa mikwaju ya penati baada ya matokeo ya sare ya agregate ya mabao 2-2
Mechi hii ya nusu fainali inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa, huku RS Berkane wakitumia faida ya uwanja wa nyumbani na uzoefu wao katika michuano ya Afrika, wakati CS Constantine wakilenga kuendeleza mafanikio yao



